HOTUBA ILIYOTOLEWA NA MHASHAMU BABA ASKOFU MAIMBO TANZANIA NA TANGA KATIKA KANISA KUU LA KRISTO MKUNAZINI ZANZIBAR
JUMAPILI
YA KUPAA MEI 12, 2024 IBADA YA UPATANISHO
Mheshimiwa Dr. Hussein Alli Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
Mhashamu Justin, Askofu Mkuu wa Cantebury na Mwenyekiti wa Maaskofu Baraza wa Kianglikana Ulimwenguni
Mhashamu Suheil, Askofu
Mstaafu wa Yerusalem na Askofu Mkuu Mstaafu wa Mashariki ya Kati
Mhashamu Dr. Albert, Askofu wa Lusaka, Askofu Mkuu wa Afrika Kati na Mwenyekiti wa Baraza la makanisa ya Anglikana Afrika
Mhashamu Dr.Dickson, Makamu wa Askofu Mkuu Kanisa Anglikana Tanzania na Askofu wa Central Tanganyika
Mh. Shekhe Saleh Omary, Mufti wa Zanzibar
Mh. Shekhe Hassan Othman Ngwali, Kadhi Mkuu wa Zanzibar
Maaskofu, makasisi na mashemasi mliopo
Waheshimiwa Mawaziri
Waumini wetu wote
Wageni wetu wote
Waandishi wa Habari
Tunawakaribisha katika kanisa
kuu la Kristo hapa Mkunzani
Kwa wenzetu mliosafiri safari ndefu sana kutoka London, Yerusalem, Lusaka na Nairobi, tunawakaribisha sana Zanzibar. Zanzibar ni patamu, raha, na penye heri. Ukiishi katika ulimwengu huu kisha uwe hujawahi fika Zanzibar, ujue una kasoro.
Mhashamu Askofu Mkuu Suheil,
wewe ni mwenyeji wa Palestina, tunajua unakotoka kuna machafuko makubwa na
ndugu zetu wengi kule wamekufa, kwa heshima yao, na wewe mwenyewe, niombe
tusimame kwa sekunde chache.
Tumekusanyika hapa leo ili
kumletea Mungu sala na maombi yetu maana ni kwa huruma na neema zake tu,
aliiumba Zanzibar na kwa wakati aliochagua yeye, akatuma wamishenari kuja
kuujenga ufalme wake hapa.
Tupo katika kisiwa ambacho tangu karne ya saba kimekuwa kitovu cha imani na biashara. Wenzetu Waislamu ndio wa kwanza kabisa kufika hapa na wakaipanda imani yao. Ni kwasababu hii tumemualika Muft wa Zanzibar na kadhi Mkuu maana wao wanawakilisha kundi ambalo lilitupokea na kutupa ushirikiano mkubwa. Mheshimiwa Muft na Mh. Kadhi, Mungu awabariki sana. Tunamshukuru sana Mungu pamoja nanyi kwa jinsi ambavyo mmeendeleza utamaduni uliojengwa na watangulizi wetu miaka mingi iliyopita.
Historia inaonesha kwamba
wamishenari wakikristo wa kwanza kuifikia Zanzibar walikuwa Wakatoliki wakati
wakipita kwenda India mnamo karne ya 16. Ingawa wenzetu hao waliacha alama
katika visiwa hivi na kule Pwani ya Bara, lakini hawakuacha kanisa. Utume wa
Kikatoliki ulioweza kuanzisha kanisa hapa ni ule uliofika mwaka 1860
wakiwatangulia Waanglikana. Kwa heshima ya utangulizi huo, tumemwalika Askofu
wa Jimbo Katoliki Zanzibar ambae pia ni rafiki mwema sana kwa huduma hapa
Zanzibar.
Ndugu zangu maaskofu wakuu na wakuu wa nchi zetu, pamoja na Zanzibar kufahamika sana, na wenzetu wakatoliki kutangulia, historia inatutambulisha kwamba Kanisa Anglikana halikuwahi kuwa na mpango wa kuanzisha huduma Zanzibar pamoja na kwamba maeneo ya Seychelles na Afrika Kusini jirani na Zanzibar tayari kanisa Anglikana lilikuwa limejimarisha huko.
Kwa wenzetu mliosafiri safari ndefu sana kutoka London, Yerusalem, Lusaka na Nairobi, tunawakaribisha sana Zanzibar. Zanzibar ni patamu, raha, na penye heri. Ukiishi katika ulimwengu huu kisha uwe hujawahi fika Zanzibar, ujue una kasoro.
Tupo katika kisiwa ambacho tangu karne ya saba kimekuwa kitovu cha imani na biashara. Wenzetu Waislamu ndio wa kwanza kabisa kufika hapa na wakaipanda imani yao. Ni kwasababu hii tumemualika Muft wa Zanzibar na kadhi Mkuu maana wao wanawakilisha kundi ambalo lilitupokea na kutupa ushirikiano mkubwa. Mheshimiwa Muft na Mh. Kadhi, Mungu awabariki sana. Tunamshukuru sana Mungu pamoja nanyi kwa jinsi ambavyo mmeendeleza utamaduni uliojengwa na watangulizi wetu miaka mingi iliyopita.
Ndugu zangu maaskofu wakuu na wakuu wa nchi zetu, pamoja na Zanzibar kufahamika sana, na wenzetu wakatoliki kutangulia, historia inatutambulisha kwamba Kanisa Anglikana halikuwahi kuwa na mpango wa kuanzisha huduma Zanzibar pamoja na kwamba maeneo ya Seychelles na Afrika Kusini jirani na Zanzibar tayari kanisa Anglikana lilikuwa limejimarisha huko.
Mmishenari wa kwanza wa kanisa Anglikana kuifikia Zanzibar alikuwa Kasisi Johann Ludwig Krapf aliepita hapa mwaka 1844 akielekea Mombasa alikokuwa ametumwa na chama cha Kianglikana kijulikanacho kwa jina la Church Missionary Society kwenda kuanzisha huduma huko Mombasa.
Tukio lililopelekea Zanzibar kupokea Uanglikana lilianzia na kifo cha Askofu Charles Richard Mackenzie, askofu wa kwanza wa chama cha kiangliaka kijulikanacho kwa jina la Universities Mission to Central Africa (U.M.C.A) ambae mwaka 1862 alipata maralia kali akiwa safarini mto zambezi na akafa na kuzikwa huko. Tukio hilo pamoja na kukwama kwa kazi katika milima ya Shire huko Malawi, lilipelekea UMCA kujiondoa huko kwa nia ya kwenda Natal Afrika Kusini kujipanga upya.
Wakati wanakatiza mkondo wa Mto Zambezi kuingia Bahari ya Hindi, Askofu George Tozer aliemrithi Mackenzie, akiwa na rafiki yake Kasisi Edward Steer, jahazi lao lilivumilishwa na upepo wa Monsoon na kuwaswaga hadi hapa mwaka 1864. Kwa hiyo ujio wao haukuwa wa mpango bali wa Roho Mtakatifu mwenyewe.
Mhashamu Askofu Mkuu Justin, tunajua unaijua historia hii maana imeandikwa vizuri katika vitabu vyetu. Sababu ya kuirudia hapa ndio umuhimu wa siku hii na kwa kweli, tunamshukuru Mungu kwamba wewe binafsi, askofu Mkuu Albert na Suheil mmeweza kufika. Tunasikitika tu kwamba Askofu Mkuu Thabo wa Afrika Kusini ambae kanisa lake ndio lilimtoa Askofu Mackenzie na akawekwa wakfu huko Cape Town hakuweza kuungana nasi leo. Kwa wale msiojua, Askofu Mkuu Thabo asili yake ni Zanzibar hivyo tunasikitika kutokuwa nae leo.
Wahashamu Maaskofu wakuu na Waheshiwa wageni wetu, Askofu Tozer alipofika hapa tunapoabudu leo palikuwa soko kuu la kuuzia ndugu zetu waliochukuliwa utumwani kutoka nchi ambazo leo ni Zambia, Tanganyika, Malawi, Rwanda, Burundi na DRC.
Pale juu ilipo madhbahu ndipo ilipokuwa nguzo ya kuwafunga na kuwapiga watumwa walioonesha upinzani wowote ule. Mtumwa wa aina hiyo alifungwa pale, akapigwa sana mbele ya wote ili kuwaonesha wengine kwamba hawana uhuru. Pale ndugu zetu walitandikwa mijeredi, walitemewa mate na wangine walibamizwa kwa makofi.
Askofu Tozer alipokelewa vizuri sana maana tayari Zanzibar ilikuwa na balozi mdogo wa Uingereza ambae alikuwa na urafiki wa karibu sana na Sultan wa Zanzibar ambae wakati huo tayari amejimilikisha visiwa vyote na kutawala sehemu kubwa ya Tanzania Bara. Askofu Tozer alipokwenda kujitambulisha, Sultan alitaka kujua kwanini wazungu wale wako Zanzibar. Askofu alijibu kwamba amefika Zanzibar kuitangaza dini ya nabii Ibrahimu.
Sultan
ambae nae alikuwa mfuasi wa dini ya Kiislamu ambayo ina mizizi yake katika dini
hiyo ya Ibrahimu, alifurahi na kwa hiyo akampatia zawadi ya watumwa vijana
watano (Swedi, Feruzi, Farijallah, Songoro and Mabruki).
Sultan pia aliwakodisha wamishenari wetu jengo la kuanzia shughuli zao ambalo leo linaitwa Mambomsije na ibada ikaanza hapo tarehe 4 Septemba 1864 waafrika wa kwanza wakiwa zawadi iliyotolewa na Sultan kwa misheni. Mambomsije kwa sasa ni hoteli ya kitalii na chumba kilichokuwa chapel ndio kina bei kubwa zaidi kwa sababu ya historia hii.
Sultan pia aliwakodisha wamishenari wetu jengo la kuanzia shughuli zao ambalo leo linaitwa Mambomsije na ibada ikaanza hapo tarehe 4 Septemba 1864 waafrika wa kwanza wakiwa zawadi iliyotolewa na Sultan kwa misheni. Mambomsije kwa sasa ni hoteli ya kitalii na chumba kilichokuwa chapel ndio kina bei kubwa zaidi kwa sababu ya historia hii.
Wahashamu Maaskofu Wakuu na wageni wetu, hii ndio historia inayobeba sababu za uhusiano mwema uliojengeka kati ya Waislamu na Waanglikana na Kanisa na serikali hapa Zanzibar. Uwepo wa viongozi wetu wa kitaifa hapa leo umejengwa katika msingi huu ambao, tunamuomba Mungu asiibuke mtu hata mmoja wa kuutikisa kwa namna yoyote ile.
Wahashamu Maaskofu Wakuu na wageni wetu, katika msingi huo kanisa Anglikana liliendelea kujiimarisha hapa Zanzibar hata kuyafikia maeneo ya Msumbiji, Malawi, Zambia, na sehemu kubwa ya Tanzania Bara. Kutoka hapa pia chama ca CMS kilituma wamishenari kwenda Uganda na hatimae kuifikia Rwanda na Burundi na DRC. Wamishenari walitumia njia kuu tatu:
Kwanza, walinunua watumwa na kuwabatiza,
Pili pale ambapo hawakuwa na fedha walivamia majahazi yaliyobeba watumwa na kuwateka.
Njia ya mwisho waliyotumia ni kuiiba watumwa na kuwabatiza.
Familia ya ya Kihindu ya Jairam Senji, mmoja wa wafanyabiashara tajiri
Zanzibar wakati huo na ambayo ilikuwa ikimiliki nyumba moja kubwa hapa na eneo
la wazi la kutunzia watumwa, ilitoa nyumba hiyo na sehemu hiyo kuwa zawadi kwa
misheni. Kanisa Anglikana Tanzania, linaishukuru sana familia ya Senji na West
kwa heshima waliyoipa Kanisa la Zanzibar. Leo tumemualika mmoja wa wanafamilia
wa Senji ili kuishukuru familia hii kwa mara nyingine.
Lakini pia shukrani zetu
uzipokee wewe Mhashamu Askofu Mkuu Justin kwa jinsi ambavyo kanisa lako
lilikusanya fedha kwa haraka sana na kuweka jengo hapa la kipekee kabisa kwa
ukanda huu wa Afrika. Jengo hili la mtindo wa Basilika iliyotengenezwa kwa
kuchanganya utamaduni wa kigothiki na kiarabu ni urithi wa kipekee sana. Kama
tulivyoeleza mwanzoni kwamba hata ile madhbahu pale ilipo imebeba heshima ya
kipekee sana na ujumbe ambao huukuti popote katika kanisa hapa duniani. Ni pale
pale walippopigwa ndugu zetu, ndipo Kristo ajitoapo kwa ajili yetu akitujia
katika fumbo la mkate na divai.
Ni palepale ambapo damu za ndugu zetu
zilimwagika, ndipo tubarikipo divai kuwa damu ya Yesu Kristo, ni palepale
walipouzwa wasiokosa, ndipo ajitoapo mwanakondoo wa Mungu ili auponye
ulimwengu. Natamani theolojia hii ambayo
hatuna kanisa jingine popote duniani isambae kotekote iwalete mahujaji hapa,
wajue jinsi Zanzibar ilivyo kuu na utukufu. Katika ubeti wa 4 wa Nyimbo za Dini
499 mwandishi anakamata wazo hili:
Ubeti wa sita wa wimbo huo
huo nao ubeba shangwe ile ile:
Twapenda meza ile
Tukuonapo, Bwana
Hapana kama hapa
Popote duniani
Twapenda
kuziimba
Rehema tupewazo
Twataka kuzijua
Wanazoimba juu
Ndio maana sisi wengine
tunapata taabu sana kusikia wako wanaochezea mahali hapa na kupafanya kama ni
mahali pa mchezo mchezo tu. Kama kuna mahali posipopaswa kuchezewa ni mahali
hapa. Kwasababu ya upekee wa mahali hapa na ile tarehe 6 juni, tunaleta ombi
kwa kanisa na serikali. Tarehe 6 Juni ndio siku ambayo Mkataba wa Kukomesha
biashara ya utumwa ulitiwa saini hapa Zanzibar. Nionavyo mimi hii ndio siku ya
uhuru wa Afrika. Nionavyo mimi hii ndio siku tukufu kabisa ya kuenziwa.
Mheshimiwa Rais, ukiona vema, siku hii ipewe heshima kwa kufanya makongamano ya
kitaifa kuhusu ubaya wa baiashara hiyo na kukemea machipuko mengine ya biashara
ya binadamu.
Inaweza pia kutumika kutengeneza kufufua njia walizopita watumwa na kuweka kumbukumbu za bandari walizoingizwa katika majahazi kule Bara. Nauona mradi mkubwa kabisa wa kiimani, kitalii na kibiashara. Ama kwa upande wa kanisa, tunatangaza rasmi kwamba tarehe 6 Juni itaingia katika kalendari yetu nasi tutakuwa hapa kila tarehe hiyo kufanya adhmisho katika kanisa hili. Ngoja tuanze tu kwa uchechefu, mema yatakuja mbele ya safari.
Wahashamu Maaskofu Wakuu na wageni wetu, kusainiwa kwa mkataba wa kukomesha biashara ya utuma kulileta changamoto kubwa mbili kwa misheni ya kanisa hapa Zanzibar. Kwanza, watumwa waliokuwa njiani kuja hapa na wale waliokuwepo tayari hakukuwa na pakuwapelekeka. Misheni ilichukua hatua za haraka kwa kuchangisha fedha ilikununua maeneo ya kuwatunza. Mashamba makubwa ya Buguruni Malapa na Mtoni Shamba (Dar es salaam), Mbweni, wete na Kiungani (Zanzibar), Kilimatinde (Singida), Berega (Morogoro), Mpwapwa (Dodoma), Masasi (Mtwara) na Magila na Misozwe huko Tanga yalinunuliwa na Kanisa la Uingereza. Kwa mara nyingine tunashukuru sana Kanisa la Uingereza kwa kusudi la kuwatunza watumwa waliokombolewa.
Changamoto ya pili ambayo iliikumba misheni hapa Zanzibar ni jinsi ya kuwatunza hawa watumwa waliokombolewa. Kwa kuwa fedha hazikutosha, misheni ilianzisha shughuli za kujitegemea. Shughuli kama vile kilimo, kuchoma chokaa, kupasua mawe, ujenzi na shughuli za ndani zilianza katika vijiji hivi vipya vya kikristo.
Hata hivyo,
kwa kuwa wana vijiji hawa waliishi maisha ya utumwa hapo kwanza, wakajikuta wamisheni
wanawatumikisha watu hawa kama watumwa tu. Waliamshwa kabla jua kuchomoza kwa
ajili ya sala na misa, kisha ikafuata usafi na kisha kazi na kufuatiwa na sala
nyingi na kazi. Hapa ndipo ilizaliwa
falsafa ya kazi na sala.
Mateso yalikuwa makubwa maana kila aliekosa kusali
aliadhibiwa sawa na ambae hakufanya kazi yake sawasawa. Waliopinga jambo hili
walifukuzwa na mmoja wa waliofukuzwa ni miongoni mwa wale vijana watano wa
kwanza aliopokea Askofu Tozer. Zaidi ya hayo, kwa kuwa UMCA ilizuia wamishenari
kuoa au kuolewa, baadhi ya wamishenari wasiojiheshimu walifanya zinaa na wana
vijiji hawa wapya na ilipogundulika wamishenari walifukuzwa ila hawa watoto na
wazazi wao wakawa mali ya misheni.
Wamishenari wakajipatia
heshima hata kuwaita watu hawa waliokuwa wakiwatumikia kuwa ni wa kwao. Maneno
kama vile my boy, my girl, tone boy yanayoonesha umiliki wa watu hao wakati
ule. Hali ilivyokuwa katika vijiji vya
Kikristo ndio pia iliyokuwa kwa watumwa waliokuwa wanafanyakazi katika mashambani
na nyumba za wenzetu waarabu na wahindi.
Mtumwa aliekuwa mgonjwa hakuwa na maana aliekuwa mzima ndie alihitajika sana. Mateso haya yalijenga utegemezi ambao hata leo bado ungali ukiitafuna nchi yetu. Wako watu leo anapomuona mtu mweupe kutoka Ulaya anafikiri ameona Mungu. Wako watu hata wanaogopa kujiita wamezaliwa na watu waliokuwa watumwa na hata wengine wanataka habari hizi zisisimuliwe kana kwamba hakuna kilichotokea maana kwao utumwa ni udharirishaji mkubwa. Kwa kuwa hakuna popote katika historia Kanisa liliomba radhi kwa wazanzibar na nchi zilizotoa watumwa, nikuombe Mhashamu Askofu Mkuu Justin, wakati wa hotuba yako, useme neno kwa niaba ya nchi yako na kanisa.
Majahazi yaliyobeba watumwa
yaliyofika jioni sana yalishusha watumwa na wakafungiwa katika mapango kumi na
mawili yaliyokuwa katika jengo letu hapo nje (tumebakisha mapango mawili baada
ya kufukia mengine yote wakati wa ujenzi. Hali ilivyokuwa katika mapango
inasikitisha: Padre Steer anaeleza jinsi hali ilivyokuwa: “niliona watumwa kwa
maelefu wamelala chini wamechoka sana, wengine wana vidonda miguuni na wengine
majeraha midomoni, pengine kwa kupigwa huko njiani.
Wengi wao wamefungwa
minyororo na magongo shingoni ili wasitoroke. Inasikitisha sana kuoa hali hii.
Asubuhi waliletwa kuuzwa kwa mnada na wakasafirishwa kwenda Uarabuni baada ya
kulipiwa ushuru kama bidhaa vile.” Walipofika huko wanaume walihasiwa ili
wasije wakazaa na wake za mabwana wao. Wanawake wengi waligeuzwa kuwa watumwa
king’ono. Waliopata mimba kwa bahati mbaya waliuawa kwa kificho. Kisa kimoja
kilichoandikwa kinaonesha mwanamke mjamzito alieuwa na kupasuliwa ili watoto wa
bwana wake waone jinsi mtoto anavyoishi tumboni. Matendo haya mabaya yasiyo ya
utu, yametendwa kwa ndugu zetu. Waliotenda hawapo tena, ila sisi tupo hivyo ni
kuombe Mhashamu Suheil wakati ukisimama useme neno la msamaha kwa makosa haya
ya kibinadamu.
Kana kwamba hiyo haitoshi, wakoloni walihakikisha waafrika wote wenye uwezo wanawaua. Walimnyonga mtemi wa Wasambaa kule mazinde, wakamua chifu wa Wachaga kule Moshi, wakawaua Bwana Heri kule Tabora wakati wa Vita vya Pangani, waliwaua wapiganaji wa vita vya ukombozi vya MajiMaji kule songea, wakamsaka Mtemi wa wahehe na kuepelekea kifo chake kule Iringa. Walipoona wamewanyamazisha Waafrika, wakaanza kuchukozana na kugombana wao kwa wao na mwaka 1914 Vita Kuu vya kwanza vya Dunia vikaanza kupiganwa katika nchi yetu. Ndugu zetu walibebwa kwenda kupigana vita ambayo haiwahusu, wengi walikufa kwa vita na maslahi yasiyo yao. Wamishenari wetu wote walisombwa wakapakiwa katika malori na gari moshi wakaenda kufungwa Kiboriani Mpwapwa na hatimae wakapigwa kifungo kibaya gereza la Tabora. Walimu wetu waafrika 55 walitembezwa kwa miguu kutoka Tanga mjini hadi Rufiji kupitia handeni, Kiteto, Kondoa, Dodoma na Morogoro. Wengi walikufa njiani kwa njaa na vipigo, wengine wakafa maji katika mto Rufiji walipokuwa wanajaribu kutoroka hata waliorudi wakabaki 11 tu. Padre Petro Limo akiwa gerezani aliteswa hadi jicho likapofuka na mkono mmoja ukapooza. Padre Cecil Majaliwa nae alifungwa gerezani mwaka mzima bila chakula na maji isipokuwa uji tu. Padre Sehoza anaeleza katika kitabu chake “Mwaka katika Mnyororo”
jinsi alivyonyanyaswa gerezani wakati ule. Baada ya vita hivi kwisha viliibuka vita kuu vya pili ambavyo vilipelekea ndugu zetu kwenda kupigana katika nchi za mbali kama vile Bangladeshi na Pakistani. Wengi walifia huko katika vita isiyowahusu. Tunamshukuru Mungu kwamba wakati wa ziara yake mwaka 2023, Rais wa Ujerumani aliomba radhi kwa watanzania. Kwa kuwa taifa la Uingereza halijawahi kutengeneza jambo hili, kupitia misa hii, nimuombe Mhashamu Askofu Mkuu Justin aseme neno kwa Watanzania nikijua kwamba Ubalozi wa Uingereza nao unasikia na utachukua hatua kama hiyo.
Pamoja na madhira haya, sasa umeibuka utumwa mpya tena, vijana wetu kutoka nchi zile zile wakisakwa kwa ahadi za kazi huko ulaya, uarabuni na hata humu humu nchini. Biashara hiyo haramu ya watu kwa jina jipya Human Trafficking imetengenezwa kimtindo kiasi kwamba ni vigumu kuing’amua kwa haraka. Wanajihusisha na biashara hii wanatumia ombwe lililopo la kutokuwepo ajira kama kigezo. Serikali yetu inajitahidi sana kuwashika wale wanaopitia hapa. Hata hivyo shughuli hiyo imelekea magereza yetu kulemewa mno na wahamiaji haramu. Gharama ya kuwatunza watu hawa ni kubwa mno. Nitumie fursa hii kumuomba Mhashamu skofu Mkuu Justin, kutumia uwakilishi wetu kuishawishi UN ione jinsi ya kuisaidia Tanzania kubeba mzigo huu. Pia tuwatake waumini wetu na wenzetu waislamu, tushirikiane kukomesha biashara hii maana wanaofanya biashara hii wengi ni waumini wetu na wanaleta sadaka.
Lakini pia hapa Zanzibar mara kadhaa tumesikia baadhi ya wenzetu wa imani ya Kiislamu wakitaka kila mtu atiii kutokula mchana wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Jambo hili ni baya kwasababu kwa nchi ambayo haina dini na inaheshimu dini za wengine, utalazimishaje kila mtu afuate dini yako? Ni jambo baya pia maana nchi yetu inategemea sana utalii, tukishaanza kuwabagua watu kwa dini zao, tutajikuta tunawapoteza watu hao. Kanisa linaishukuru sana serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Ofisi ya Mufti kwa kukemea jambo hili ambalo likiachiliwa lina madhara makubwa.Ni imani yetu viongozi wetu mtaendelea kulipiga vita jambo hili.
Mhashamu Askofu Mkuu Justin, tupo mahali hapa ambapo pia mtu aliefanya kazi kubwa ya kukiandika Kiswahili kwa herufi za Kiingereza amelala kanisa hili. Huyu sio mwingine bali Askofu Edward Steer aliemrithi George Tozer. Askofu Steer ndie mtu wa kwanza kuandika kamusi ya Kiswahili –kiingereza, wa kwanza kutoa Litujia kwa Kiswahili, wa kwanza kufasiri Injili zote nne kwa Swahili. Ni yeye pia aliejenga kanisa hili na yuko hapa amelala. Naamini ananisikia, ngoja nimwite Edward,
Tunakukumbuka leo kwa kazi yako. Jambo linalotusikitisha Mhashamu Askofu Mkuu ni hili, wakati kanisa lako liliwekeza fedha nyingi hapa kukifanya Kiswahili kiwe hivi kilivyo leo, ila hatuoni kikitumiwa katika makutano makuu ya kanisa badala yake tunasikia Kiingereza, kireno na Kifaransa zaidi kaa kwamba Mungu anazungumza lugha hizo tu.
Tunashukuru kwamba kwa mara ya kwanza mlitupa nafasi kuongoza misa kwa Kiswahili katika mkutano mkuu wa kanisa ulimwenguni ujilikanao kwa jina la Lamberth Conference mwaka 1978 na 2021. Tunashukuru kwamba kwa mara ya kwanza Mkutano wa Maaskofu wakuu tumetoa misa kwa Kiswahili kule Rome mwaka huu. Hata hivyo, Kiswahili kinachotumika humo ni cha wenzetu wakenya na wakonga. Tulisikitika hata katika mkutano wa Kanisa Ulimwenguni mfasili hakukuwa na mtanzania hata mmoja. Pengine ofisi ya ACO haijui kwamba kuna utani huku kwamba Kiswahili kilizaliwa Zanzibar, Kikaendeezwa Tanganyika, Kikajaribiwa kuzungumzwa Kenya, kikauawa Uganda na DRC wakakizika kabisa. Sasa unawatumiaje watu waliozika lugha kufanya tafsiri? Tutumie fursa hii kuiomba ACO ishirikiane na Baraza la Kiswahili Zanzibar na Tanzania kuinua Kiswahili katika ulimwengu wa Kianglikana.
Watu waliokaribu na mbali
Watu wajinga
na wenye elimu,
Wanadamu wa kila taifa
Ndie
mwenyezi anaewatunza
Watu
maskini na watu wakubwa
Watu weusi na watu
weupe
Wana
wafalme na wana watumwa
Watu
wamoja machoni pa Mungu
Askofu William
alijitahidi sana kuirudishia Zanzibar heshima yake lakini haikuwa rahisi.
Kwanza, aliona ilikuwa muhimu kumleta Askofu Msaidizi kuiandaa Zanzibar irudie
heshima yake na kwa hiyo akamwekea mikono Kasisi Neil Russell kuwa askofu mwaka
1963 na kumtuma hapa. Kama alivyokuwa Frank, Russell nae alikuwa mchungaji
mwema sana. Siku zote aliwatembelea Rais Karume na waumini nyumba kwa nyumba
kujua taabu zao. Katika wajibu wake huo, aligundua kwamba waumini wake wanaume
waliokuwa wanafanya kazi serikalini walikuwa na nyumba ndogo na hawakuwa
wanajali matunzo ya familia zao.
Askofu Russell akawaita mmoja mmoja na kuwaonya
jambo ambalo wazee hao na nyumba ndogo hawakutaka na hivyo wakaweka kichungo na
kumshitaki askofu kwa Rais kwamba anapinga Mapinduzi na Africanisation. Askofu
ambae alitoa kanisa hili kuendesha vikao vya siri kuelekea mapinduzi, na ambae
alimsindikiza John Okelo na Sultan hadi Dar es Salaam ili kuinusuru Zanzibar
mara baada ya mapinduzi, akaamriwa aondoke ndani ya masaa 24 mwaka 1964. Askofu
aliondoka hadi bandarini na pale alikimbizwa na walinzi waliokuwa wamepewa amri
na serikali na hapo akaacha viatu vyake. Neil Russell ambae ndie amefungua makanisa
kideleko, Mombo, Mazinde, Kihurio, Mnazi, Mwala na Vunta huko Bara siku zote
ametembea miguu peku na alipoulizwa sababu za kufanya hivyo alisema viatu vyake
walimnyang’anya wazanzibar.
Baada ya
Russell kundolewa Zanzibar kwa fitina za wazee Askofu William aliamua
kuiunganisha Zanzibar na Dsm na hivyo ikaanzishwa Dayosisi ya Zanzibar na Dsm
mwaka 1964 lakini nayo haikudumu maana ilivunjika mwaka uliofuata tu kwa hiyo
Zanzibar ikapelekwa Tanga ikajulikana kuwa Daysosisi ya Zanzibar na Tanga tangu
mwaka 1965 chini ya William. Yohana Jumaa aliemrithi William tangu 1968,
hakuthubutu kurejesha kiti cha Zanzibar hadi alipoingia John Ramadhani ambae
nae jitihada zake tangu mwaka 1980 hazikufanikiwa hadi mwaka 2000 ndipo
akafanikiwa na kuirudishia Zanzibar kiti chake ila fimbo ilibaki Dsm.
Askofu
John alifanikiwa kuiongoza Zanzibar pengine kwa kuwa anatoka katika ukoo
mkubwa. Yeye alirithiwa na Douglas Toto ambae nae alipitia shida nyingi hadi mauti
ya ghafla ilipomkumba. Baadhi yenu mtakumbuka maneno yake katika Kanisa la Mt.
bartholomayo Ubungo Dsm siku chache kabla ya kifo chake. Baada ya kifo cha Douglas Dayosisi ilikosa
askofu kwa miaka 8 ndipo akachaguliwa Michael ambae nae hajamaliza vizuri.
Nimetumia muda mrefu kueleza hapa kwasababu naona yako mambo hayako sawa katika
kiti cha uaskofu wa Zanzibar. Nitumie fursa hii kuomba radhi kwa Askofu Frank,
Masista wa CSP, Askofu Thomas Birley, Askofu William Scott Backer, Neil
Russell, Askofu Douglas Askofu Michael na makasisi Thomas Godda, John Mwamazi
na Noel Ndahani kwa yote waliyopitia hapa. “Ee
Mungu usikiaye kuomba, wewe ambae wote wenye mwili watakujia, usiyakumbuke
makosa yetu, wala makosa ya baba zetu, wala usitupatilize kwa dhambi za watu wako,
utuachilie Bwana mwema, utuachilie sisi watu wako uliotukomboa kwa damu yako ya
thamani na kwa hiyo usituonee ghadhabu.Ni wewe tu Bwana wa kukifungua kiti cha
uaskofu wa Zanzibar, fungua ili kanisa lako lipone. Amin.
Wahashamu Maaskofu Wakuu na wageni wetu, ninapoelekea mwisho wa hotuba yetu, hebu sasa tuigeukie Biblia. Katika Biblia kipo kisa cha majibizano ya Yesu Kristo na Masadukayo kuhusu kama ilikuwa halali kumpa Kaisari kodi. Katika kisa hicho Yesu aliwaomba wampe dinari na alipoishika akawageukia akawauliza, sahihi na sanamu iliyokuwa juu ya dinari ilikuwa ya nani na wawakamjibu ni ya kaisari. Yesu akawaambia basi mpeni kaisri iliyo haki yake na Mungu haki yake(Math.22:15-21).
Nichukue fursa hii kuomba tena Mungu atusamehe kwa wizi huo. Bahati mbaya sana, hakuna shughuli yoyote ya kijamii ambayo unaiona hapa ikifaywa kwa kutumia fedha hizo maana ingelikuwepo tungelikuwa na udhuru kwa serikali.
Kwa kuwa tumeiba vyakutosha na kwa kuwa hatuwezi kurudisha tulichoiba, nitumie fursa hii kumuomba Mh. Rais wa Zanzibar kwanza atamke neno la kutusamehe kabisa kabisa na irekodiwe vizuri. Pili tumuombe achukue hatua madhubuti ili serikali ipate haki yake na kanisa lipate haki yake hapa. Tatu tumuombe alihakikishie kanisa kwamba shughuli hiyo ya kupata kodi kutoka hapa haitaathiri shughuli za kanisa wala kuingilia uhuru wa ibada na hiyo nayo irekodiwe vizuri.
Mwisho na sio kwa umuhimu, naleta mamobi yafauatayo kwa serikali yetu na kwa kanisa la Uingereza:
1. Kwa kuwa Juni 6 ndio siku mkataba wa kukomesha biashara ya utumwa ulipotwa saini hapa Unguja na biashara hiyo kuharamishwa kabisa, napendekeza siku hii ipewe hadhi yake. Mheshimiwa Rais, mkiona vema tungeweza kufanya kazi jambo hili na mimi naona fedha itakayokuja hapo baadae sisi tukiwa hatupo. Naiona fedha ndefu hapa kama tukiiundia miundo mbinu. Ziko shughuli ambazo hazijafanywa vyakutosha. Professor Shimvji anasema kweli kwamba eneo la historia ya shughuli za dini na maingliano yake na serikali yakifanyiwa tafiti vizuri, yanaweza kuwa chanzo kikubwa cha mapato ya serikali na sisi tunaona ukweli huo kwa kuanzia na jambo hili.
3. Kwa kuwa ziko kelele nyingi kuhusu ajira kwa vijana wa Kikristo kutopewa nafsi, tunaishuri serikali ilifanyie kazi jambo hili kuleta usawa na kupunguza kelele.
No comments:
Post a Comment