Social Icons

Pages

Featured Posts

Saturday, November 11, 2023

CHUO KIKUU MZUMBE WATETA NA WANAJOGGING TANDALE

 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu Mzumbe Dkt. Godbertha Kinyondo na Mtafiti Chuo Kikuu Mzumbe Aloyce Gervas wakikabihi jezzi kwa wanakikundi cha Five Star Jogging 
cha Tandale akipokea ni Mwenyekiti wa Five Star Jogging Tandale, Ramadhani Abdala Juma.


Mhadhiri wa Chuo Kikuu Mzumbe Dkt. Godbertha Kinyondo akizungumza leo Novemba 10, 2023 wakati wa kutoa elimu juu ya Hifadhi za jamii kwa wafanyakazi wa sekta zisizo rami kwa wanakikundi cha Five Star joggin kilichopo Tandale jijini Dar Es Salaam.
Mtafiti Chuo Kikuu Mzumbe Aloyce Gervas akizungumza na akizungumza leo Novemba 10, 2023 wakati wa kutoa elimu juu ya Hifadhi za jamii kwa wafanyakazi wa sekta zisizo rami kwa wanakikundi cha Five Star joggin kilichopo Tandale jijini Dar Es Salaam.
Mwenyekiti wa Five Star Jogging Tandale, Ramadhani Abdala Juma akitoa shukurani kwa wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe kwa kuwapa Jezi ambazo watazitumia kufanya mazoezi nakuhamasishana kuwa na maadili mema.

Picha za pamoja.


Wanakikundi cha Five Star Jogging Tandale wakijaza fomu kwaajili ya kujiunga na Mfuko wa Hifadhi za jamii wa NSSF

Wafanyakazi wa NSSF wakitoa elimu kwa Wanakikundi cha Five Star Jogging Tandale 


Matukio mbalimbali.

Na Mwandishi wetu.
UELEWA mdogo ma kipato kidogo, vimetajwa kuwa ndio changamoto ya watu wasio katika mfumo rasmi wa ajira kujiunga na mifuko ya hifadhi za kijamii pamoja na bima za afya nchini.Hayo yamesemwa na Mhadhiri na mtafiti wa Chuo Kikuu Mzumbe, Dkt. Godbertha Kinyondo leo Novemba 10, 2023 wakati wakitoa elimu kwa vijana kikundi cha mikimbio mwendo (Jogging) ya Five Star iliyopo Yemeni Tandale wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa Chuo Kikuu Mzumbe Kinatoa Elimu kupitia tafiti iliyofanyika katika nchi tatu ikisusisha Chuo cha Nairobi nchini Kenya, Chuo Kikuu Mzumbe na Roskilde.


Amesema utafiti huo ulijikita katika huduma ambazo Wajasiliamali wadogo wanatakiwa kuchangia ambazo ni Pensheni za Mifuko wa Hifadhi za jamii (NSSF), Bima ya Afya, Mikopo ya Biashara ya Benki na Saccoss, Mafunzo ya Veta, NIT na Polisi. Pamoja na huduma ya Ushirikishwaji wa Vikundi, vyama vya wafanyakazi...

Amesema kuwa Kikundi cha Five Star Jogging hawana uelewa kuwa wanaweza kupata Pensheni ya Uzeeni kwani wanajua kama Pensheni inapatikana kwa Wafanyakazi wa Serikalini tuu, hivyo katika kuwapa elimu baadhi ya wanakikundi hicho wamejaza fomu kwaajili ya kuanza kuchangia.

"Sisi Chuo Kikuu Mzumbe katika Utafiti wetu tumeenda mtaani kabisa kuangalia hawa watu wanajikimu namna gani na namna ambavyo wanaweza kujikimu katika maisha yao. Mzumbe tumeazimia kwenda Mtaani, Mtaa kwa Mtaa kuamsha watu kuhusu hizi hifadhi za jamii." Amesema Dkt. Kinyondo.

Makundi ambayo yameshafikiwa ni Wajasiliamali wadogo, Bodaboda, Makondakta, Wajenzi, Mama Ntilie na vikundi vya Jogging.

Akito ushauri kwa NSSF, amesema kuwa watumie ukuaji wa teknolojia katika kutoa huduma ili kuondoa usumbufu kwa jamii pale inapofatilia Mafao yao pale wanapohitaji mafao au wanapostaafu na nguvu kupungua.


Pia amewaasa wana Kikundi cha Tandale Five Star Jogging kukata bima ya Afya ili iweze kuwasaidia pale waapata Changamoto za kiafya.

Dkt. Kinyondo ameeleza kuwa nchi inapoenda kuwa na bima ya wote, ni wajibu wa kila mwananchi kujibidisha kushiriki kwani kuna nchi ambazo zilishatekeleza mpango huo mfano Rwanda na Ghana. Hata hivyo ni asilimia isiyozidi 60 wamejiunga huko Ghana, na Rwanda ni kama 80 wamejiunga.

Hivyo elimu inahitajika kwa wananchi kupokea mpango wa Bima ya afya kwa wote. Ila katika tafiti imegundulika kwamba wafanyakazi wa sio katika sekta rasmi muda wao ni kutafuta kipato hivyo hawataki urasimu kwenye huduma. Hivyo utegemea zaidi kulipa fedha toka mifukoni huko hospitali wakiamini ukiwa na hela unatibiwa haraka kuliko ukiwa na bima.

Pia wamelalamikia suala la kukosa dawa hospitali pale wanapopata huduma kwa kutumia bima ya afya.

Akizungumzia kuhusiana na kuwekeza amesema Uwekezaji katika mfuko wa UTT unafaida kwani unaweka fedha na pia unapata faida. Amesema kuwa vikundi vingi walivyovifikia, vimeweza kujiunga na UTT na ameshauri kikundi hiki kujiunga na mfuko huo, jambo ambalo wamekubaliana kulishughulikia hilo wiki ijayo.

Kwa Upande wa Mtafiti Kutoka Chuo Kikuu Mzumbe, Aloyce Gervas amewakumbusha kudumisha umoja walionao ili kuwezakufika mbali ikiwa pamoja na kuomba mikopo mbalimbali itakayowawezesha kufanya biashara.

"Kidole Kimoja hakivunji Chawa ushirikiano ni mzuri na unaleta maendeleo kwa haraka zaidi kuliko ukiwa peke yako," amesema Aloyce.

Amesema amewaasa kuheshimiana wawapo kwenye kikundi wadumishe upendo na ushirikiano hapo hakuna kitu kinachoharibika na ili kikundi kisonge mbele.

Licha ya Kutoa elimu kuhusu Mifuko ya Kijamii Wametoa jezi za Kikundi chao ambazo watatumia wakati wa kufanya mazoezi.

Licha ya hayo Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Tafiti amesema watawafikia vikundi vingine ambavyo vitakuwa balozi wa kueneza hifadhi za jamii kwa wananchi katika maeneo wanapoishi.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Five Star Jogging Tandale, Ramadhani Abdala Juma amewashukuru Chuo Kikuu Mzumbe kwa kuwapa Jezi ambazo watazitumia kufanya mazoezi na kuhamasishana kuwa na maadili mema.

Amesema kuwa changamoto kubwa ilikuwa ni namna ya kupata bima za afya na Mifuko ya Pensheni. "Hivyo basi wametupa elimu ya namna ya kujiunga na mifuko ya kijamii na bima ya afya katika vikundi vidogo vidogo tulivyonavyo, jambo jingine ni kutokujua kama wanajogging pia wanaweza kupata Pensheni Uzeeni pamoja na bima ya afya."

Pia amewaahidi Chuo Kikuu Mzumbe kuzitumia Jezi hizo kwa maadili bila kuaibisha nembo au Chuo Kikuu Mzumbe.

Wednesday, November 8, 2023

TRA KUANZA KUWASHUKURU WALIPA KODI

 

Mkurugenzi wa Elimu kwa mlipa kodi na mawasilano TRA, Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa Habari makao makuu ya ofisi zao jijini Dar es Salaam leo Novemba 8, 2023 kuhusu wiki maalum ya kuwashukuru na kuwapongeza walipa kodi kwa hiari na wakati itakayoanza Tar 18 hadi 24 siku ya kilele chake.


MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) leo Novemba 08, 20223 imeanza Wiki ya shukrani kwa mlipakodi ambapo itatambua walipakodi wao waliofanya vizuri katika mwaka wa fedha wa 2022/23.

TRA hutumia wiki hiyo kuwatambua wale waliolipa kodi kwa hiari na wale waliotoa ushirikiano wa kutosha kulipa kodi lengo ni kuwatia hamasa walipakodi wote waliolipa kodi zao kwa hiari, bila kusukumwa wala kufuatwa fuatwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano, Richard Kayombo amesema kuwa kilele cha wiki hiyo ni Novemba 24, mwaka huu itakayofanyika Mlimani City, Dar es Salaam na mgeni rasmi atakuwa Naibu Waziri Mkuu, Dotto Biteko.

Sambamba hilo, matukio yatakayotangulia kuelekea kilele ni kuwepo kwa shindano la vilabu vya kodi kwa shule za Sekondari za Dar es Salaam na Pwani ambapo shule 59 zitashiriki.

"Hawa ni wale walipakodi waliotoa ushirikiano kwa maofisa wetu ikiwemo kutoa taarifa za ukaguzi na hata ritani pale walipohitajika. Kimsingi hawa ni wale waliotekeleza sheria ya kodi," amesema Kayombo.

Kayombo amesema lengo ni kuhakikisha wanajenga uhiyari wa kulipa kodi kwa vijana wadogo ili wanapokuwa watu wazima wawe walipakodi wazuri.

Amesema vijana hao wanapaswa kufahamu umuhimu wa kulipa kodi kwani wapo watakaokiwa wafanyabiashara, wakandarasi na wafanyakazi ndani ya TRA.

"Tukio la pili ambalo tutalifanya ni matembezi na mbio za shukrani kwa mlipakodi hivyo vikundi mbalimbali vinakaribishwa," amesisitiza.

Pia ameeleza kuwa siku ya kilele watakuwa na makundi ya kitaifa ikiwemo ya washindi, makundi ya kisekta na makundi ya Wilaya na Mikoa lengo kuzingatia kila kundi la mlipakodi.

Amesema mwaka wa fedha uliopita, makundi mbalimbali yalipata tuzo hizo na mshindi wa jumla alitoka kwenye sekta ya fedha na kwamba walipokea maswali mengi kutoka kwa walipakodi kwanini hawakutajwa kwenye tuzo hizo.

Amefafanua kuwa kwa mwaka huu wanaamini watu wengi wanazidi kuhamasika ili waweze kutambulika kwa kazi nzuri ya kulipa kodi, pia kuwaletea heshima na kuaminika kwa wateja wao.

Ameeleza kuwa kaulimbiu kwa mwaka huu ni Kodi yetu, maendeleo yetu, tuwajibike ikilenga watu walipe kodi, wadai risiti wafanyapo manunuzi na kutoa taarifa ya wanaokwepa kodi.

Monday, March 21, 2016

WANAFUNZI WASOMEA CHINI KWENYE UDONGO HUKU WAKIFUNDISHWA NA MWALIMU MMOJA.

Na Woinde Shizza,Simanjiro
MPANGO mkakati wa elimu bure kuanzia darasa la Awali mpaka Sekondari umeonekana kutonufaisha baadhi ya walengwa katika maeneo ya pembezeno hususani jamii ya kifugaji  kutoka katika kijiji cha Kichangare wilayani Simanjiro Mkoani Manyara ambapo wananchi wameamua kumkodisha mwalimu na kumlipa kwaajili ya kufundisha watoto wao.

 Wanafunzi wa shule hii ya msingi Kichagare  wamekuwa wakijisomea huku  wamekaa chini, shule hiyo ikiwa imeezekwa  na vipande vya turubai ili kuweza kupata afueni wakati wakujisomea ambapo lengo la wazazi wao kufanya hivyo ni kuwasaidia watoto wao kupambana na adui ujinga ili kuendana na karne hii ya sasa ya teknolojia.

mwandishi wetu amebahatika kufika eneo la tukio na kuzungumza na mwalimu wa shule hiyo aliyejitambulisha kwa jina la  Lilian Nanyaro ambapo amesema kuwa aliamuakujitolea kufundisha katika shule iliyoko kijiji cha Kichangare kitongoji cha Loongung  hii ikiwa ni kwa ajili ya kuweza kuwapatia wanafunzi na watoto wa kijiji hicho elimu .

Amesema kuwa  mazingira ya shule ya msingi Kichangare ni magumu haswa katika swala zima la ufundishaji kwa hamna vitendea kazi ndani ya shule hiyo ukizingatia  kwamba watoto ambao  ni wanafunzi wana nia ya kutaka kusoma.

‘’ndugu mwandishi kama mnavyoona mazingira ya shule hii yaliyomagumu hamna paa, paa lililopo ndo hivi vipande vya turubai na mengine yametuboka  na pia ukiangalia mazingira ya kijiji chetu mvua zinaponyesha pia inakuwa ni tatizo kubwa sana kwani  inafikia mahali  wanafunzi hushindwa kufika shule kabisa nanapenda kutumia nafasi hii kuomba mbalimbali kuweza kutusaidia tatizo hili kwani iwapo watoto hawa watapata sehemu nzuri ya kusomea itawasadia sana hivo  wadau wajitokeze kutusaidia’’alisema Nanyaro.

Kwa upande wake mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo amejitambulisha kwa jina la Seigulu James  amesema kuwa wao kama wanafunzi wanatamani sana kusoma lakini tatizo kubwa walilonalo katika shule hiyo ni madawati hawana, kwani  kwa sasa iviwamekuwa wakikaa chini wakati wakiwa wanasoma.

Ametumia fursa hiyo kuiomba Serikali kuwasaidia kuweza kupata angalau madawati pamoja na kuwajengea majengo ya madarasa pamoja na kuwapatia walimu ambao wataweza kuwafundisha ili waweze kupata elimu kama wanafunzi wengine na  watoto wa shule  zingine.

Honie Kimbeye Mkazi wa kijiji cha Kichangare wilayani Simanjiro amesema kuwa wao kama wanakijiji waliamua kukaa na kutafuta mwalimu mmoja ambaye ndio wanae hapo shule ambapo amesema wao kama wanakijiji wanajichangisha ela na kumlipa mwalimu huyo ili aweze kuwafundisha watoto wao.

“sisi tulijikusanya tuka kaa tukaona ni bora tutafute mwalimu ambaye atatusaidia kufundisha watoto wetu hapa kijijini hivyo tunajichanga tunamlipa kila mwisho wa mwezi na kila mzazi amekuwa akichangia shilingi elfu nne kwa ajili ya kumlipa mwalimu huyo”alisema Kimbeye

Kwa upande wake afisa mtendaji wa kata ya Loongung Japhet Losijake amesema kuwa mapaka sasa  tayari  vikao vyao vya bajeti halmashauri wameshaomba kijiji hicho kipewe kipaumbele ili kuweza kuondoa tatizo la ukosefu wa darasa hali inayowafanya watoto kusoma wakiwa chini ya vumbi.

Wahenga wanamsemo usemao usipoziba ufa utajenga ukuta,hivyo ni vyema kama serikali kwa kushirikiana na wizara ya elimu kuangalia eneo hilo kwa ukaribu ili kuweza kuwaondolea changamoto hiyo inayowakabili wanafunzi n ahata mwalimu kufundisha katika mazingira magumu.

MWANAMKEMMOJA ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KOSA LA MAUAJI YA KIKATILI.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma Zubery Muombeja.

MWANAMKE mmoja aliyejulikana kwa jina la Frida Kapinga mkazi wa Mkuzo kata ya Msamala mjini Songea  mkoani Ruvuma anashikiliwa na jeshi la Polisi mkoani humo kwa kosa  la kufanya mauaji ya kikatili dhidi ya mtoto wake wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu.

TAMASHA LA PASAKA MWAKA HUU KUKEMEA MAUAJI YA VIKONGWE NA ALBINO.

MBUNGE wa Viti maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),UPENDO PENEZA amesema kuwa ni uamuzi mzuri uliochukuliwa na kampuni hiyo kwani mkoa huo umekithiri kwa mauaji ya vikongwe na watu wenye ulemavu hivyo ni ishara kubwa ya kuelekea kukombolewa.

Peneza alisema kuwa anaamini watu wakimpenda Mungu wataacha kufanya mauaji ya vikongwe na albino na watu wa kawaida, kwani mkoa huo unaongoza kwa mauaji ya aina hii.Alisema Tamasha hilo ni msaada mkubwa kwa mkoa huo kwani litahamasisha na kupinga mauaji huku akisisitiza kuwa kampuni ya Msama ambayo inasifika kusaidia jamii anaiomba pia iwafikie hata watoto wa mitaani wa mkoa wa Geita.

“Tunamshukuru Msama na kamati yake kwani Tamasha linaweza kuwa msaada mkubwa kwa mkoa wetu mauaji yamezidi si kwa walemavu wa ngozi na vikongwe hata watu wa kawaida wanauwawa kwa mapanga na vitu vingine” alisema Peneza.Alitolea mfano wa mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa mkoa wa Chadema, Alfonce Mawazo aliyeuwawa kwa kukatwakatwa mapanga hivyo kupitia tamasha la pasaka litawaasa waache mauaji.

“Kupitia hili Tamasha naamini wataacha vitendo hivyo kwa sababu Mungu anasema tusiue, mpende mwenzio, kwa hiyo mimi nadhani tamasha hili liwe la kihistoria kwa ajili ya kuwataka na kumrudia mungu,” anasema. Peneza alisema asiwe Msama tu hata asasi, kampuni na wadau mbalimbali wajitokeze kupinga mauaji kwani hilo ni janga la kitaifa.

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI ATEKELEZA AGIZO LA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM PAUL MAKONDA LA KUHAKIKI SILAHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia kwa makini zoezi la uhakiki wa silaha zake lililokuwa likifanywa na Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Neema Laizer Ikulu jijini Dar es salaam. Mhe. Rais amekuwa mtu wa kwanza kutekeleza agizo la Mkuu wa Mko wa Dar es Salaam Paul Makonda.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam Kamishna CP Simon Sirro kulia akimkabidhi Silaha aina ya Bastola Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya uhakiki uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam Kamishna CP Simon Sirro kulia akimkabidhi silaha aina ya shortgun Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya uhakiki uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiiweka silaha yake vizuri mara baada ya kuhakikiwa Ikulu jijini Dar es Salaam.

KUMBUKUMBU YA MIAKA 5 YA MZEE JOHN LUWANDA

Baba wa Mzee BEDA
 
 
Blogger Templates